Ombi la mdaiwa
- Mdaiwa atawasilisha taarifa kuhusu mali zake Mpokeaji Rasmi kabla ya kufungua Ombi mahakamani.
- Mpokeaji Rasmi atatoa hati ya kukiri kupokea na kuiwakilisha Mahakamani.
- Mahakama ikiridhika itatoa amri ya Upokeaji na Mpokeaji Rasmi anakuwa Mpokeaji aliyeteuliwa.
- Mpokeaji Rasmi ataendelea chini yaSheria ya Ufilisi, Sura ya 25 Toleo la 2002 na kufilisi mali ya mdaiwa.
Ombi la Mdai
- Mdai atafungua ombi mahakamani kupata amri ya kufilisi mali ya mdaiwa.
- Mpokeaji Rasmi atatoa hati na kuwasilisha mahakamani.
- Mahakama itatoa amri ya Upokeaji na Mpokeaji Rasmi anateuliwa kuwa Mpokeaji.
- Mpokeaji Rasmi ataendelea chini ya Sheria ya Ufilisi, Sura ya 25 toleo la 2002 na Kanuni zake kufilisi mali ya mdaiwa.

